Jaji ajiondoa katika kesi iliyowasilishwa na CORD

Na, Sophia Chinyezi
Jaji wa Mahakama Kuu, George Odunga amejiondoa katika kesi iliyowasilishwa na muungano wa CORD kuhusu zabuni ya ukaguzi wa sajili ya wapigakura iliyopewa kampuni ya KPMG.

Tume ya Uchaguzi IEBC awali ilimtaka Jaji Odunga kujiondoa katika kesi hiyo kwa kuwa huenda uamuzi wa hivi punde kuhusu zabuni ya uchapishaji ya karatasi za kura, ambayo walipoteza, huenda ukaathiri uamuzi wa kesi hiyo.
Kupitia wakili Wambua Kilonzo, IEBC vilevile imewasilisha ombi jingine la kumtaka jaji huyo kuiwasilisha kesi hiyo kwa Jaji Mkuu ili abuni jopo la kuisikiliza kesi hiyo.

 

Related Topics

George Odunga IEBC