Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands Daily
★★★★ - on Play Store
Download App

Polisi watoa tahadhari ya shambulizi la Kigaidi wakati wa Krismasi

Na Maganga

Wananchi wametakiwa kutahadhari kufuatia uwezekano wa kushuhudiwa kwa mashambulizi ya kigaidi wakati wa sherehe za krismasi na mwaka mpya. Idara ya usalama nchini imesema kwamba wanampango wa Al Shabaab na wale wa kundi la IS wanapanga kuyashambulia maeneo ya mpakani, Kaunti ya Mombasa vilevile magari ya uchukuzi wa umma.
Kulingana na Inspekta Mkuu wa Polisi Joseph Boinnet, Kundi la IS limekuwa likiendeleza usajili wa vijana nchini kwa lengo la kuwatumia kutekeleza mashambulizi. Katika taarifa, Boinett amesema kundi la Al Shabaab kwa upande wake limekuwa likijigawanya kwa vikundi na kupenyeza maeneo ya Mandera, Wajiri, Garissa na Lamu.
Amesema washukiwa wa kundi hilo wamekuwa wakitumia fursa ya mvua inayonyesha kuingia nchini hasa maeneo ya Kolbio Kaunti ya Garissa. Vilevile baadhi ya washukiwa wamekuwa wakidai kuwa wafugaji na kutafuta fursa ya kuingia nchini kutoka Somalia huku wengine wakitaka kuingia kupitia msitu wa Boni. Hata hivyo amesema usalama umeimarishwa katika maeneo yanayolengwa na magaidi.
Onyo hilo limejiri wakati ambapo mafisa wa kukabili ghasia pamoja na wenzao wa kitengo cha RDU wamenusurika kifo baada ya kilipuzi kilichotegwa ardhini kulipuka katika barabara ya Elwak-Dabacity, kaunti ya Mandera.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902