Na Beatrice Maganga
Rais Uhuru Kenyatta ametimiza ahadi yake ya kupunguza msongamano katika magereza ya humu nchini ili kisiwapo kisingizio cha kutohukumiwa kwa wahusika wakuu wa ufisadi kwa madai ya kukosekana kwa nafasi za kuwazuilia. Rais ametangaza kuachiliwa huru kwa wafungwa elfu saba waliohukumiwa kwa makosa madogo madogo na waliokuwa karibu kukamilisha vifungo vyao.