Safaricom yaagiza fidia kwa wateja

Na, Beatrice Maganga
 
Safaricom yaagiza fidia kwa wateja
 
Kampuni ya Mawasiliano ya Safaricom imeiagiza Kampuni ya Challa Communications kuwafidia wateja wake kima cha shilingi bilioni 10.6 walizotozwa walipotuma ujumbe mfupi wa kupokea matokeo ya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane, KCPE.
Safaricom imesema baadhi ya waliotuma ujumbe huo walitotwa ada zaidi bila kukusudia na wanastahili kurejeshewa fedha zao.
Kampuni ya Chala ni miongoni mwa zinazofanikisha huduma za mawasiliano. Safaricom aidha imeagiza kufidiwa kwa wateja ambao walituma ujumbe lakini hawakupata ujumbe wowote kuhusu majibu ya mtihani huo. Kila ujumbe uliotumwa kwa nambari 22252 uligharimu shilingi 25. 

Related Topics