Anasema mwimbaji maarufu kutoka nchini Tanzania, Mrisho Mpoto, kuwa ukikanyagwa maksudi kwenye sherehe ya harusi huambiwi pole, lakini kwenye tafrija za matanga huambiwa samahani!
Kauli hiyo hapo juu yaendana sambamba na jinsi hali ilivyokuwa nchini Kenya mwaka jana, punde tu baada ya kutangazwa matokeo ya mtihani wa taifa wa darasa la nane, KCPE, sawia na matokeo ya mtihani wa taifa kidato cha nne, KCSE.