Acres of maize destroyed - Swahili

Mvua kubwa iliyoandamana na tufani imesababisha hasara kubwa kwa wakulima huko eldoret ya mashariki. Zaidi ya hekari mia sita za ngano na mahindi zimeharibiwa na mvua hiyo, na kuwaacha wakulima wakikadiria hasara. Hofu kubwa ni kwamba huenda wakakabiliwa na janga la njaa, hasa ikizingatiwa kuwa tangazo la idara ya utabiri wa hali ya anga nchini, limesema kwamba ukame unaozidi kushuhudiwa humu nchini utaendelea kwa muda.