Drought update - Swahili

Huku baa la njaa likiendelea kuangamiza watu wengi humu nchini hasa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano na wakongwe, serikali na mashirika mengineo yamelaumiwa kwa kubagua maeneo ya kutoa chakula cha msaada. Hata hivyo katibu mkuu wa shirika la Red cross Abbas Gullet amewahimiza wafadhili kuendelea kutoa misaada yao kwani idadi ya wale wanaoathirika na baa la njaa ingali iko juu.