Mystery Uni student murder

Habari zinazozingira kifo cha Mercy Chepkosgei Keino aliyekuwa akisomea shahada uzamili katika chuo kikuu cha Nairobi zinaendelea kujitokeza. Huku polisi wakiendeleza uchunguzi rafikize Mercy waliokuwa wamemwalika katika sherehe hiyo nyumbani kwao huko Westlands wanadai mwendazake aliondoshwa mara mbili na walinzi baada ya kuvunja glasi katika nyumba hiyo. Maafisa wa polisi wamemhoji mbunge wa Juja William Kabogo anayedaiwa kuhudhuria sherehe hiyo. Johana Chacha na ripoti kamili.