Building demolition-Swahili

Idara ya wahandisi nchini IEK imesema baraza la jiji la Nairobi ndilo la kulaumiwa kutokana na mikasa ya hivi punde ya kuanguka kwa majumba katika maeneo ya Nairobi. Idara hiyo imesema mikasa hiyo ingezuiliwa iwapo baraza lingefuata mapendekezo ya mwaka 2006 ya jopo la wahandisi lililoundwa baada ya mkasa wa nyamakima uliosababisha zaidi ya vifo vya watu kumi na tano.