Death at kakamega mines - swahili

Watu watatu walifariki huku wengine watatu wakinusurika kifo  baada ya maji kufunika mgodi wao eneo la kakamega. Wachimbaji hao wa dhahabu katika migodi ya rosterman walikumbwa na mkasa huo baada ya mto mmoja ulio karibu na mgodi wao kuvunja kingo zake na kufunika mgodi huo. Juhudi za maafisa wa idara ya kushughulikia mikasa ya manispaa ya kakamega kuwaokoa walionaswa katika mgodi huo hazikufua dafu kwani waliwasili katika eneo la mkasa bila ya vifaa vinavyohitajika