Maafisaa wa shirika la wanyama pori nchini wamemuua kwa kumpiga risasi mshukiwa mmoja mwindaji haramu katika mbuga ya solio ilioko laikipia mashariki. Bwana huyo alikuwa miongoni mwa wenzake watatu wanaodaiwa kuingia kinyemela katika mbuga hiyo jana usiku kwa nia ya kuwawinda vifaru weusi ambao kwa sasa wanasemekana wamebaki mia sita na thelathini tu katika mbuga zote nchini.