Mauaji Ya Kutatanisha Kinale

Maafisa wa polisi tena wapo matatani baada ya maiti  kumi na nne ya watu waliopigwa risasi kupatikana katika msitu wa kinale. Watu hao kumi na wanne mara ya mwisho inasemekana walitiwa nguvuni na maafisa wa polisi na kisha miili yao kupatikana ikiwa na majeraha ya risasi.Aidha waliweza kuwasiliana na jama wa kabla ya mauaji hayo kutelekezwa na kudai kwamba walikuwa wamezuiliwa katika kituo cha polisi cha kinale.Maiti hizo kwa sasa zipo katika hifadhi ya maiti ya city baada ya kusafirishwa na maafisa wapolisi wa kituo cha lari.