Mzozo Wa Mpaka Tharaka Tigania

Taharuki   na ukosefu wa usalama unazidi kutanda  miongoni mwa jamii  zinazoishi mpakani mwa tigania na tharaka huko Meru; na hata kupelekea vifo vya watu sita kufikia sasa.Waziri wa usalama George Saitoti  amefanya ziara katika eneo hilo kwenye juhudi za kujaribu kuhubiri amani bila ufanisi mkubwa. Mshukiwa  mmoja ameshatiwa nguvuni kufuatia   uhasama baina ya jamii hizo uliopelekea mamia kuhama makwao.