×
App Icon
The Standard e-Paper
Truth Without Fear
★★★★ - on Play Store
Download Now

NHIF yatangaza mabadiliko kadhaa katika utoaji wa huduma kwa wateja

Katika hatua ambayo inatarajiwa kuibua hisia mseto miongoni mwa Wakenya, Hazina ya Kitaifa ya Bima ya Afya, NHIF imetangaza mabadiliko kadhaa chini ya bima hiyo kukiwamo kupunguzwa kwa idadi ya watoto wanaonufaika na kadi ya wazazi wao kutoka kumi hadi watoto watano.

Mabadiliko hayo ambayo yalianza kutekelezwa tarehe mosi mwezi huu aidha yanamwidhinisha mke mmoja tu kunufaika na huduma za afya chini ya kadi moja.

Uamuzi huo uliafikiwa katika kikao maalum cha bodi ya NHIF tarehe 17 mwezi Desemba mwaka uliopita ambapo iliafikiwa kwamba iwapo familia itakuwa na watoto sita na zaidi, watano tu ndio watakaonufaika na bima hiyo huku waliosalia wakitakiwa kuongeza kiwango cha fedha wanazolipa kila mwezi.

Aidha, wanaokosa kulipa ada ya kila mwezi kwa kipindi cha miezi 12, uwanachama wao utafutiliwa mbali na kutakiwa kujisajili upya, hali inayomaanisha kwamba ataweza kuanza kunufaika na huduma hizo baada ya siku 90 baada ya kujisajili upya.

Get Full Access for Ksh299/Week
Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in

Related Topics