Katika maelezo ya historia ya watu wa Mijikenda, tumesikia kwamba kulikuwa na watu waliokuwa na vipawa mbali mbali na pia majikumu tofauti tofauti. Wazee wa Kaya, walikuwa makuhami ambao ndio waliokuwa na majukumu ya kuliongoza taifa kwa njia nyingi.
Wazee hawa ndio waliokuwa na majukumu ya kufanya maombi kwa niaba ya jamii nzima, ila tu walipotoka kufanya maombi hayo, walikuja kuwaeleza watu yale maagizo waliyopewa kutokana na maombi yao. Mengi ya waliyoamriwa kufanya kama jamii, yalifuatwa bila ya maswali kutoka kwa jamii, kwani, hawa ni watu waliokuwa na uwezo wa kuzungumza na ‘Mulungu’ na mara walipopewa maagizo ya kufuata, basi kila mtu alikuwa hana budi kuyafuata maagizo hayo.