PNU, ODM wapooza moto 9/04/09

Hali ya vuta ni kuvuta inayokabili Serikali ya Muungano ya Kenya sasa inaonekana kupungua huku viongozi wa PNU na ODM wakitaka masuala nyeti ya muungano huo kujadiliwa kwa njia ya amani. Muungano wa PNU pia umekatiza maandamano yaliyotarajiwa kufanyika kote nchini, huku Rais Kibaki akiwataka viongozi kujiepusha na uchochezi. Aidha wanachama wa ODM William Ruto na Joseph Nyaga wametoa mwito kwa Raila Odinga kujihusisha na mazungumzo ya amani ili kusuluhisha mzozo katika  Serikali ya Muungano.