Leo hii tunasherehekea mashujaa waliopigania uhuru wa nchi yetu Kenya. Mashujaa ambao walijitoa kihali na mali kuhakikisha kwamba tunajitawala kivyetu vile tupendavyo. Japokuwa matamanio ya wazee hawa yaweza kuwa hayajaafikiwa mia fil mia, ni vyema kuwapongeza kwa kazi yao shwari.
Kazi yao ilitufanya kuabiri magari sawa na watu wa matabaka tofauti tofauti na hata watu wa rangi mbali mbali bila kuwazia atokako mtu. Yaani kwa ushujaa wao wa kukubali kuishi msituni kulikokuwa na hatari mbali mbali kama vile wanyama pori na baridi kali ya kufanya mtu azizime.