Kutoka sare 0-0 nyumbani dhidi ya washindani wao wakuu Mathare United mwishoni mwa wiki kumeharibu mfululizo wa matokeo mema ya Bandari ilotazamiwa kushinda na kudhibiti nafasi ya kwanza kikamilifu katika jedwali la ligi kuu nchini KPL.
Mkoko ndio mwanzo umealika mauwa kwani songmbwingo ya ligi imechacha na kuzidi kuchacha.Kila timu inajituma pakubwa kuandikisha matokeo mema.