Wetangula Dhidi Ya Natembeya: Bora Kwa Demokrasia Ila Sio Kwa Vurugu
Published Mar. 27, 2024
00:00
00:00

Ubabe wa kisiasa kati ya Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetangula na Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya ni dhihirisho la demokrasia ya nchi. Hata hivyo, ubabe huu haufai kuishia kuwa wa vurugu. Sepetuko inakariri kuwa kamwe vurugu hazifai kuwa sehemu ya siasa za taifa hili. Wanaohusika katika kuzua vurugu mazishini, kwenye mikutano ya hadhara au kwingineko kokote kule lazima wawajibishwe kisheria.