Shule nyingi nchini zinaendelea kufanya kazi huku zikiwa na idadi ndogo ya wanafunzi, na baadhi zikiripotiwa kutokuwa na mwanafunzi hata mmoja. Hali hii imeisukuma Wizara ya Elimu kuanza kuzingatia mpango wa kuziunganisha shule hizo na kuhamisha walimu kwenda katika taasisi zinazohitaji zaidi.
Katika ukaguzi wake wa hivi majuzi, wizara imebaini kuwa zaidi ya shule 6,000 zina wanafunzi chini ya 100, huku shule 10 za upili zikifungwa baada ya uchunguzi kubaini kutokuwa na wanafunzi kabisa. Hili limeibua maswali kuhusu uwezekano wa matumizi mabaya ya fedha za umma.