Rais William Ruto ameweka wazi kwamba yuko tayari kwa mazungumzo na Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga.
Hata hivyo, Rais Ruto ambaye amezungumza katika Kaunti ya Bomet wakati wa uzinduzi wa barabara ya kilomita 75, amesema kuwa hawezi kukubali vitisho vya Azimio kukiwamo kurejelea maandamano ya kila wiki Jumanne ijayo.