Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Fearless, Trusted News
★★★★ - on Play Store
Download App

Abraham Serem Ateuliwa kuwa Kaimu Afisa Mkuu Mtendaji wa KenGen

Abraham Serem ndiye Kaimu Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya KenGen baada ya kuteuliwa kushikilia wadhifa huo. Serem anachukua nafasi hiyo kutoka kwa Rebecca Miano ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Maeneo Kame na Maendeleo katika Maeneo.

Katika notisi iliyochapishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Kengen, Samson Mwathethe kwenye magazeti ya humu nchini leo hii, imesema kwamba Serem atahudumu katika wadhifa huo hadi wakati mtu mwingine atakapoteuliwa kwa wadhifa huo.

Serem amekuwa akihudumu katika wadhifa wa Meneja Mkuu vilevile mkuu wa wafanyakazi tangu Machi mwaka 2016. Ana tajriba ya miaka 20 katika kitengo cha kuwahudumia wafanyakazi, HR.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902