Ziwa Nakuru ni maarufu kwa maelfu ya ndege aina ya flamingo, na ndicho kivutio kikubwa cha watalii nchini Kenya lakini katika miaka ya hivi karibuni, kupungua kwa idadi ya ndege hao kumeshuhudiwa, ambapo wataalamu wanasema hali hii imesababishwa na ongezeko la maji ziwani humo na kuchangia ukosefu wa chakula. Kwa sasa wanasayansi wameanzisha mchakato wa kutafuta chakula mbadala kuwasaidia ndege hao aina ya flamingo.