Premium

Sonko aapa kumsaidia Conjestina tena

Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko amejitolea kwa mara nyingine kumsaidia aliyekuwa mwanandondi Conjestina Achieng, baada ya picha ya Conjestina maarufu Conje, kusambaa mitandaoni na kuibua hisia za kuhuzunisha.

Katika Mtandao wa Twitter, Sonko amesema tayari ametuma gari  moja hadi nyumbani kwa Conjestina ili kumsafirisha hadi Mombasa kwa ajili ya maombi.

Sonko amedokeza kwamba ameshauriana na familia ya Conjestina, kwamba bondia huyo aliyeiletea Kenya sifa mara kadhaa, apelekwe Mombasa kufanyiwa sala katika kanisa moja baada ya kukosa kupata nafuu alipotibiwa hospitalini.

Kulingana na Sonko, mwana wa Conjestina Charlton Otieno ndiye aliyemwona usaidizi akisema familia ya Conjestina inakumbana na matatizo ya kifedha licha ya kuwahi kuwa mashuhuri na kuiletea Kenya sifa.