×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Watu watatu wafariki katika ajali ya barabara Bomet

19th August, 2018

Watu watatu wamepoteza maisha yao katika ajali mbaya ya barabarani iliyotokea katika eneo la Kamureito kwenye barabara ya kutoka mjini Bomet kuelekea Kaplong.

Abiria wengine kumi na tisa walijeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali za Kaplong na Tenwek kupokea matibabu.

Taarifa zinasema kuwa matatu hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria kumi na nne pekee ilikuwa imebeba jumla ya watu 21 wakati wa ajali hiyo.

Walioshuhudia wanasema kuwa gari hilo lilibingiria mara kadhaa baada ya gurudumu kupasuka. 

 

.
RELATED VIDEOS