Chama cha wazazi nchini kimewataka walimu kutoongeza karo ya ziada wiki hii wanafunzi wanapofungua shule kwa muhula wa pili.
Mwenyekiti wa chama cha Wazazi tawi la Homa Bay Julius Omuga, amehofia kwamba huenda baadhi ya walimu wakuu wakaongeza karo licha ya muhula wa pili kuwa mfupi.
Akiongea na Radio Maisha kwa njia ya simu, Omuga amewataka walimu kukamilsha silabasi vyema bila kuwaongezea wazazi gharama yoyote.
Aidha amehimiza walimu kuzingatia viwango vya karo vilivyoidhinishwa na Wizara ya Elimu.