Hali ya mkanganyiko wa hisia imeshuhudiwa nyumbani kwa Tom Okwach mmoja wa wachimba migodi waliofukiwa na mchanga wakiwa hai ndani ya chimbo la Abimbo, katika Kaunti ya Siaya baada ya mwili wake kupatikana miezi saba tangu alipotoweka.
Familia ya marehemu imesema imefurahi kupata mwili wa mpendwa wao licha ya kujawa na huzuni wakati mabaki ya mwili huo yalipokuwa yakitolewa.