Mabadiliko ya baraza la mawaziri ya Rais Uhuru Kenyatta yanaendelea kupokelewa kwa mikono tofauti na hisia mbali mbali haswa baada ya kumtimua kazi waziri wa Kilimo, Mwangi Kiunjuri.
Nafasi yake imechukuliwa na Peter Munya. Kiunjuri amefungashwa kuelekea nyumbani wakati wizara yake inazuzushwa na Nzige ambao wanaendelea kuvamia maelfu ya mimea na mazao kaskazini mwa Kenya.