Huku mizozo ya ardhi ikiendelea kutafutiwa suluhu kwa udi na uvumba, hasa eneo zima la Pwani kwa ujumla, swala hilo limechukua mkondo mpya baada ya familia moja kutoka Utange kaunti ya Mombasa kulalamikia mawakili wao kunyakua ardhi ambayo walikuwa wanawawakilishia kesi yao ya shamba la ekari kumi katika kijiji cha Maweni sehemu ya Shanzu eneo bunge la Kisauni.
Walalamishi Mzungu Chengo na Thoya Chengo mwenye umri wa karibu miaka 58 na Bahati Thoya Kamandi, wanadai ndio wamiliki halisi wa kipande hicho cha ardhi ambacho waliachiwa na Mhindi zaidi ya miaka 22 Sasa.