Muungano wa waalimu nchini KNUT umejulikana kwa mda mrefu kama muungano wa kutetea msalahi ya wanachama wake kwa ari na nguvu ya kipekee kutokana na wingi wa wananchama wake ambao ni walimu wa shule za msingi na baadhi ya wale wa shule za upili.
Maafisa wake wakuu ambao wamekuwa wakichaguliwa ndani ya fani ya ukufunzi, ama waliokuwa walimu kwa wakati mmoja, wameonakana kunoa makali kila kuchao kukabiliana na muajiri wa waalimu wa shule za umma ambayo ni Tume ya kuajiri Waalimu TSC.