Hofu imeanza kuwaingia wafuasi wa chama tawala cha serikali cha Jubilee katika kaunti ya Mombasa kufuatia ilani kutoka kwa mwenye jengo linalositiri afisi za chama tawi la kaunti kwamba nyumba inauzwa. Jengo hili ambalo limo katika maeneo ya Tudor, yakadiriwa mwenyewe anataka kuliuzwa kwa jumla ya shilingi 60 milioni.
Hii inamaanisha kwamba chama cha Jubilee katika kaunti ya Mombasa lazima kigurishwe (kuhamishwa) hadi kwa makao mengine licha ya kuwa kitaifa, kimeanza kuteteleka. Ingawa hivyo, baadhi ya wafuasi wa Jubilee wa kaunti wanachukulia hatua na msukumo wa kuuza jengo hili lenye afisi za chama kuwa njama fiche ya kisiasa kutaka kuaibisha chama hiki cha serikali. Kodi ya nyumba hii imekuwa ikilipwa na mratibu wa chama jimbo la pwani, Farid Swaleh.