Hali inabashiria kwamba huenda kukawa na makundi mawili yanayoorodheshwa kuwa ya MRC lakini likawa moja la kundi ‘A’ likawa lile rasmi la kina Omar Mwamnuadzi na lingine la ‘B’ ambalo uhai wake ni wa kusadikika tu kufuatia matukio sawa ya uvamizi wa vijana ulioripotiwa juzi na idara ya polisi katika kaunti ya Kilifi.
Muda mfupi tu baada ya taarifa za vijana wanaosemekana walikuwa wanachama wa kundi la MRC kuponyea chupu kwenye msitu wa Jibana ambapo kulingana na taarifa za polisi, ilibainiwa kuwa zaidi ya vijana 50, Pambazuko ilijaribu kuchimba uwezekano huo kutaka kujua kutoka kwa baadhi ya viongozi wake lakini wakakana vikali kwamba vijana hao kamwe hana uhusiano wowote na MRC ambayo inaangazia haki yake kisheria.