Diwani wa zamani Choi Keronche alishangaa alipotembelea mji wa Kisii miaka minne iliyopita baada ya kuwa jela kwa miaka 22 jela kwa kosa ambalo anasema kamwe hakulitekeleza. Diwani Keronche aliona jinsi mji wa Kisii ulivyokuwa na majumba makubwa akilinganisha na wakati alipokuwa huko mara ya mwisho mnamo miaka 1990 kabla yeye na nduguye mdogo Francis Chweya kujipata kizimbani wasijue kuwa wangetoka huko wakiwa hai.