Siku chache baada ya baraza kuu la chama cha ODM kumtimua mbunge wa Malindi Aisha Jumwa Karisa, mbunge huyo ameukosoa utaratibu uliotumiwa na kamati kuu ya chama hicho kumtimua chamani.
Akiongea huko Malindi baada ya kulakiwa na wafuasi wake waliokuwa wamebeba mabango yenye maandishi ya “tulimchagua kiongozi wala sio chama,” amesema hakubaliani na uamuzi huo, kwani sheria na taratibu hazikufuatwa hivyo yeye bado ni mbunge wa Malindi kwa mujibu wa Katiba.