Wakaazi katika eneo la Takaungu kaunti ya Kilifi wanaendelea kutofautiana kuhusina na ujenzi wa kituo cha kuhifadhi gesi, kwa madai kuwa kujengwa kwa kitua hicho kutasababisha uharibifu wa mazingira.
Baadhi ya wakazi hao wanasema hawataruhusu kituo hicho kujengwa eneo hilo wakidai kuwa sekta ya uvuvi ambayo ndiyo tegemeo kubwa kwa wakazi eneo hilo itasambaratika kutokana na kutupwa kwa takataka kuingia baharini.