Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia dhuluma wanazozipitia wanaume mikononi mwa wake zao katili. Hivi majuzi mwanaume mmoja kajipata matatani baada ya sehemu yake nyeti kukatwa. Kisa kingine cha hivi majuzi inatamausha kwani mwanamke mmoja kamchoma kisu mpenziwe mgongoni na pia kinena chake.Visa vingi vya aina hii inakera moyo ikizingatiwa kuwa inaenda kinyume na mantiki ya kibinadamu.
Wasemavyo weledi wa lugha, aliyeumwa na nyoka akiona ung’ong’o hushtuka.Ukweli wa kauli hii unadhihirika katika jamii zetu pale ambapo wanaume wameasi majukumu yao ya kifamilia ili kukwepa dhuluma watakazokumbana nazo.Takwimu zinaonyesha kuwa dhuluma za aina hii huchangia pakubwa na ndio msingi wa kuvunjika kwa ndoa. Aidha huwaathiri watoto ikikumbukwa kuwa wanahitaji uzazi mwema kutoka kwa wazazi wao.