Wa-Oman warudi tena kudai kodi Mombasa

Huku Wakenya wakizingirwa na jinamizi la ufi sadi usiokuwa wa kifani, jamii zaidi ya 20,000 katika mtaa maarufu wa Bondeni - Mwembekuku eneo bunge la Mvita mjini Mombasa zinakosa usingizi. Haya yanajiri baada ya kuchipuka upya kwa unyanyasaji wa vitukuu vya aliyekuwa Liwali wa kisiwa cha Mombasa Sheikh Salim bin Khalifan Abbusaid.

Mapema wiki hii ujumbe wa vitukuu hivi kutoka nchini Oman vilitarajiwa kuletwa pamoja na mkuu wa idara ya serikali kuu katika kaunti ya Mombasa, Evans Achoki kujadili kuhusu mzozo wa malipo ya kodi ya ardhi na shinikizo lao la kushurutisha jamii husika kulipa kiwango wanachotaka wao ama wauze nyumba zaidi ya 5,000 ya Wakenya ambao wameishi ardhini humo zaidi ya miaka na mikaka.

Vitukuu vya Liwali

Mchipuko mpya wa kushurutisha wenyeji wa mitaa ya Bondeni-Mwembekuku, kisiwani Mombasa kulipa ada za ajabu ulichipukia miaka miwili iliyopita katikati mwa mwezi Desemba mwaka 2017 ambapo Wakfu wa Seif Bin Salim Trust unaosimamiwa na vitukuu na vijakazi ambao walifungasha pamoja na Sultan miaka ya 1960s.

Afi si ya Wakfu huu ipo mjini Mombasa chini ya maajenti wao ambao wamekuwa wakikusanya kodi na ada za ardhi na yashangaza kwamba katika miaka ya hivi karibuni walipenya nchini na kushirikiana na baadhi ya maafi sa wakora wa ardhi kuzikatakata ardhi kadhaa kwa lengo la kuziuza pasipo kuwahusisha wakaaji wake ambao wameishi humo hata kabla ya Warabu wa Omani kuja pwani.

Katika nakala moja ambayo tumeiona kama Pambazuko kutoka kwa Wakfu wa Seif Bin Salim iliyoandikiwa mmoja wa wakaaji wa mtaa wa Mwembekuku, mnamo Desemba 14, 2017 unawaagiza wenyeji watoe malipo ya kodi ya ardhi mjini kwa kiwango cha asilimia 4% ya thamani ya kiwanja chenye nyumba zao kwa mwaka kuanzia Februari ya 2018.

Wakfu unawakilishwa na vitukuu wa Sheikh Salim bin Khalifan Abbusaid aliyekuwa Liwali wa Mombasa na ambaye ni kati ya Waomani waliojikatia ploti hizo mwaka 1908 kama cheti chake Land Titles Ordinance 1908 (East Africa Protectorate) kinavyothibitisha.

Hawatambui Kenya

Ukichunguza jinsi Waomani hawa wanavyohangaisha Wakenya kupitia kwa maajenti wao na maafi sa fi sadi serikalini, utagundua kwamba licha ya Kenya kupata uhuru miaka 56 iliyopita na serikali zote za Kenya na Uingereza kulipa fi dia zote kwa Sultan na watu wake ili kufunga virago waende, Wakenya na wenyeji halisi kama wa Mwembekuku na wengine bado wanajikuta chini ya ukoloni wa vijakazi hawa wa Oman (Absentee Landlords).

Hii inadhihirishwa na hatua ya vitukuu hawa wa Liwali Sheikh Salim Bin Khalfan kupitia kwa maajenti wa wakfu wake wa Seif Bin Salim Trust mjini Mombasa ambao umepuuza mwongozo wa serikali ya Kenya kupitia kwa tume ya ardhi nchini (National Land Commission-NLC) ambayo badala yake iliwapendekezea kukubaliana na wakaaji hao kuwauzia ploti ambazo wamejenga nyumba zao kwa kati ya shilingi laki nne hadi laki tano (400,000- 500,000) kulengana na uwezo wao.

La kuwashangaza wengi hata serikali yenyewe ya Kenya, ni vitukuu hawa ambao hakuna hata Mwarabu wao wa Oman aliyekuja hapa na ardhi kichwani ama begani ila walipatiwa ardhi ya bwerere na Sultan wa Zanzibar kwa kuwa walimtumikia kama maliwali wao. Watu hawa wanaozuru kutoka Oman, wanalazima ya kulipwa kitita cha kati ya shilingi milioni nne had kumi (4,000,000 – 10,000,000) kwa nyu ba, haijalishi hata kama ni ile ya Kiswah Wametegesha kwamba iwapo nyumb zote zaidi ya 5,000 zitatoboka kiasi hich cha pesa, wao pamoja na maafi sa wafi sa wa ardhi na wengine serikalini ambao wamewatetea kwa miaka mingi na kuwa saidia kupata vyeti gushi vya ardhi wata faidika na kuwaacha wenyeji waliozaliwa hapo kufi lia mbali na magonjwa ya mioyo.

Kodi potofu

Kulingana na mwenyekiti wa chama kinachoenzi maslahi ya wakaaji wa Mwembekuku Association Welfare-MW Mzee Abdullahi Farah anasema mtafaru baina ya pande zote mbili ulianza kujitokeza punde wenye ardhi hao kutoka Oman kutoa agizo la kuongeza ya kodi y viwanja hivyo kutoka elfu moja kwa mw (1,000) hadi kuongezeka kwa asilimia 11 hadi elfu 11,000. Anasema na hata tume NLC ilipoingilia kati, wao walidinda kufu ta muongozo wa tume. “Ole wao walifanikiwa kupata ardhi h bure wakati wa Sultan wa Zanzibar laki isiwe sababu ya kutunyanyasa sisi wanyonge ambao tulizaliwa hapa siyo kwa kimakosa ya Mwenyezi Mungu bali kwa haki zetu kama wapwani halisi”, azungumza Farah.

Rais Kenyatta saidia

Katibu wa MWA Juma Buyshenga anasema wakaaji waliokodisha ardhi hi wanaishi kwa hofu kutokana na msukum wa maajenti wa matajiri hawa wa kusadikika walio ulaya na uarabuni lakin ambao wakiota pesa usingizini, haraka hufyatuka kuwasukuma vijakazi wao ku kunyanyasa Wakenya nyumbani kwao.

“Hatuwezi kamwe kuwa na uwezo wa kulipa milioni tano kwa ploti tunazoishi. Ikiwa miongoni mwetu hatuwezi hata hicho kiwango chao cha elfu 11,000 za viwanja kwa mwezi, tutawezaje nasi maisha yetu ni yale ya lele mama,” Juma ashangaa akiongeza kuwa wengi wao hata kuezeka makuti nyumba zao kwawashinda.

Hofu ya ardhi 1962

Haya yote yanajiri miaka 56 toka Sultan wa Zandibari kulipwa jumla ya pauni mia mbili na themanini elfu 280,000 (zikaingia mfukoni mwa Sultan) za fidia, nayo serikali ya Kenya kuilipa ile ya Zanzibari pauni mia saba elfu (700,000) na kuongezewa na serikali ya Uingereza kitita kingine cha pauni milioni moja na laki tatu (1,300,000) kama fidia za kuadimika Afrika ya mashariki na vijikazi wake. Awali, Sultan huyu alikuwa ameomba makao ya ukimbizi nchini Uingereza na Saudia kwa kuhofi a kupigwa teke kwao Omani kutokana na roho yake mbaya.

Kulingana na warakha wa siri ulioandikwa na beberu mmoja kwa jina la Ian Michael Wright kwa niaba ya taasisi ya masuala ya ndani ulimwenguni wakati huo ya Institute of Current World Aff airs ya New York mnamo tarehe 15, mwezi wa Juni mwaka 1962 na kupokelewa rasmi na msimamizi wake Richard H. Nolte mnamo Juni 19, unaelezea mtazamo wa suala la vijakazi wa Sultan na ardhi kwamba iwapo Uingereza na viongozi waafrika (Jomo Kenyatta) hawataliangazia kwa makini, basi huenda tatizo sugu la wenyeji halisi wa pwani likabakia donda sugu milele.

Aliyekuwa Meya wa mji wa Mombasa Mzee Rajab Sumba atataja tatizo hili la ardhi katika kaunti ya Mombasa kama donda sugu kutoka kubanduka kwa Mkoloni. Hatahivyo anasema yungali anakumbuka wazi kuwa kabla ya Sultan wa Zanzibar kuachilia mwambao wa pwani, alitimiziwa masharti yake, kwanza, kuhakikishiwa makao yake ya ukimbizi pamoja na familia yake Uingereza na pili, kulipwa fi dia yake ili kuacha huru ukanda huu kwa wenyewe.

Kuhamia Uingezera

Katika mkutano wa kamati ya wazee wa Mombasa ulioitishwa mapema mwaka 2017 kuzungumzia suala hili, Mstahiki Rajab Sumba ananukuliwa akisema kwamba ajuavyo ni kuwa Sultan alipewa makao Uingereza na juu yake akalipwa hivyo haoni haja ya Wakenya kulipa mara mbili fungu moja la watu waliolipwa 1963. Baraza hili la Wazee wa Mombasa nalo laongozwa na mwanasiasa mkongwe Mohamed Jahazi. Maeneo mengine ambayo yanakumbwa na tatizo sawia na la Mwembekuku ni pamoja na Bondeni, Spaki, Majengo Sidiria, Sargoi, Guraya, Kiziwi na Ziwani. Kaunti nyingine za Pwani ambazo zinakabiliwa na changamoto sawa na ilivyo Mombasa, ni pamoja na Kilifi / Malindi na Lamu.