Ni asubuhi na mapema na wazee wawili wanawasili katika soko la Kiamuringa katika sehemu ya Mbeere ya kusini kaunti ya Embu wakibebamagunia mawili yaliojaa huku shamra shamra za ununuzi wa miraa aina ya Muguka ukiendelea.
Bw Njuki ambaye ni mnunuzi wa jumla wa Muguka anafungua gunia moja na kuanza kukagua miraa huku mazungumzo yakipamba moto kati yake na wazee hawa.