Uvutano wa uongozi umezidi katika chama cha FORD Kenya huku Seneta wa Bungoma Moses Wetangula akisisitiza ataendelea kuwa Kinara licha ya baadhi ya wanachama kutangaza kubanduliwa kwake.
Akizungumza na wanahabari saa chache tu baada ya kufurushwa kwake kutangazwa, Wetangula amesema mkutano uliofanywa ili kumbandua uliendeshwa kiunyme na sheria.