Kenya imeendelea kurekodi idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya korona, leo hii watu mia moja arubaini na saba wakithibitishwa kuambukziwa katika saa ishirini na nne zilizopita.
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema idadi hii kubwa mechangiwa na idadi kubwa ya sampuli zinazopimwa kwa muda uo huo. Mia moja arubaini na saba hao ni miongoni mwa watu elfu mbili mia anane thelathini na tisa waliopimwa hivyo kufikisha elfu moja mia sita kumi na nane idadi jumla ya maambukizi nchini.