Taharuki imetanda Narok baada ya mtu kuuliwa katika mapigano ya kikabila

Mtu mmoja ameuliwa huku kadhaa wakilazwa katika Kaunti za Narok na Nakuru baada ya kujeruhiwa vibaya kufuatia makabiliano makali baina ya wakazi na wezi wa mifugo.

Katika Kaunti ya Nakuru mwanamume mmoja amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Nakuru baada ya kufumwa mshale ambao umekwama mgongoni huku wengine watatu wakilazwa katika Hospitali ya Olenguruone wakiwa na majeraha mbalimbali. Wanne hao wamejeruhiwa katika makamiliano ya kikabila katika eneo la Olposimoru.

Naibu Kamishna wa Kuresoi Kusini Patrick Mwangi amesema polisi wametumwa katika eneo hilo kulinda doria .

Aidha wengine wanatibiwa katika Hospitali ya Narok baada ya kujeruhiwa katika eneo la Olowasi Narok Kusini wakati wavamizi walipowavamia wakazi na kumuua mmoja na kutoweka na ng'ombe.

Wakazi wanasema kuwa vurugu zilianza wakati watu kutoka jamii jirani walipovamia 


Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu kisa hicho huku viongozi wakishinikiza wezi hao kunaswa mara moja na kuwajibishwa