Ujumbe wa Raila Odinga kwa timu ya taifa Harambe Stars.

Kinara wa ODM, Raila Odinga ametoa ujumbe wa kuwapa motisha wachezaji wa timu ya taifa ya Harambe Stars,  baada ya kupoteza mechi yao ya ufunguzi kwenye michuano ya kuwania kombe la taifa bingwa barani afrika, AFCON dhidi ya Algeria.

Raila amewatambelea wanasoka hao kwenye kambi yao nchini Misri akiandamana na Mawaziri Amina Mohamed wa Michezo, Katibu Kirimi Kaberia na Balozi wa Kenya inchin Misri  Joff Otieno.

Raila ameipongeza Harambee Stars kwa kuonesha mchezo mzuri kwenye awamu ya pili licha ya kufanya kinyume na matarajio ya Wakenya.

Amewahimiza kutia bidii zaidi katika michuano ijayo. Amedokeza kwamba Wakenya wangali na matumaini kwamba watashinda kwenye mechi yao dhidi ya Tanzania. Kwenye mechi hiyo, Algeria ilichabanga Kenya mabao mawili kwa nunge jana usiku.

Related Topics

Raila Odinga