Sekta ya viwanda kuimarishwa kwa asilimia 15 inchini

 

Wizara ya viwanda inalenga kuimarisha sekta ya viwanda kwa asilimia 15 kufikia mwaka 2022. Vilevile mwaka jana bidhaa zilizouzwa nje ya nchi ziliimarika kwa asilimia 3.2 ambayo ni shilingi bilioni 613 kutoka shilingi bilioni 594 mwaka wa 2017.

Ripoti hiyo imetolewa na Waziri wa Viwanda, Peter Munya jijini Nairobi. Akizungumzia malalamiko ya ongezeko la raia wa kigeni katika sekta ya viwanda, Munya amesema kwamba serikali inalenga kubuni sheria ya uwekezaji  kuhakikisha kwamba raia wa kigeni hawajihusishi na biashara ambazo zinastahili kufanywa na Wakenya.

Munya amesema kwamba sheria hiyo itakayoanza mwishoni mwa mwezi Julai, itahakikisha sekta za rejareja na jumla zinaachiwa Wakenya.

Related Topics

VIWANDA SEKTA WIZARA