Sakata kuhusu biashara ya dhahabu bandia humu nchini imechukua mkondo mwingine huku Kinara wa Chama cha ODM, Raila Odinga akisema ndiye aliyefichua sakata hiyo. Raila amekiri kwamba alisafiri kuelekea nchini Dubai ili kuzungumza na mkuu wa milki za kiarabu, Sheikh Mohammed Bin Rahid Ali kuhusu suala hilo na kwamba alikuwapo wakati walaghai walipofanya mawasiliano ya simu ambayo yaliwahusisha viongozi mbalimbali.
Akizungumza katika halfa moja mjini Kisii, Raila amesema kwamba alimweleza Ali kuwa Waziri wa Masuala ya Ndani ya Nchi, Fred Matikang'i ambaye ni miongoni mwa waliotajwa kuwa ambao wangeweza kushinikiza kuachiliwa kwa dhahabu iliyonaswa asingeweza kufanya hivyo na kwamba mazungumzo yaliyonaswa kuhusu uwezekano wa watu fulani serikali kushawishi kuachiliwa kwa dhahabu hiyo yalifanywa na walaghai.