Hisia mbali mbali zinazidi kutolewa katika mitandao ya kijamii kufauatia auamauazi wa Mahakama Kuu wa kutupilia mbali kesi iliyowasilishwa kupinga sheria za Kenya kuharamisha uhusiano wa jinsia moja. Uamuzi huo umetolewa na Majaji Chacha Mwita, Roselyne Aburili na John Mativo.
Kufuatia uamuzi huo baadhi yao wakilalamika kuwa haki zao zimekandamizwa huku wengi wakiwa na mafadhaiko kufuatia ubaguzi na kunyanyaswa.