Seneta Malala apinga kuhusishna mauaji ya Matungu

Seneta wa Kakamega, Cleophas Malala amepinga vikali kuhusika katika mauaji ya Matungu na kuhusishwa na aliyekuwa Waziri wa Michezo Rashid Echesa akisisitiza kuwa yeye na Echesa hawajonana kwa muda kufuatia tofauti zao za kisiasa.

Akizungumza  wakati wa mahojiano na kipindi cha Maisha Asubuhi na Leo hii, Malala amedai kuwa kukamatwa kwake ni njia ya kufunika uhalifu wenyewe.

Amekosoa vikali Idara ya Polisi akidai kuwa wanatumiwa vibaya na baadhi ya viongozi wakuu serikalini kuwahujumu mahasimu wao wa kisiasa.

Seneta huyo ametoa wito kwa Waziri wa Masula ya Ndani ya Nchi Fred Matiang’I kuboresha usalama katika eneo la Matungu, akisisema kuwa eneo hilo halina hata kituo rasmi cha polisi.

Related Topics

malala matungu