Maseneta hawapaswi kuwashtumu magavana kufuatia ufujaji au wizi wa fedha za umma kabla hawajatathmini vyema ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali, amesema Gavana wa Pokot Magharibi, Profesa John Lonyangapuo.
Akizungumza na Radio Maisha, Lonyangapuo aidha amewasuta maseneta kwa kuhusishwa na ufisadi ilhali hawana ushahidi.