Madaktari wawili wa Cuba ambao wamekuwa wakihudumu kwenye Kaunti ya Lamu tangu mwezi Julai mwaka jana, wamehama wakihofia usalama wao, siku chache tu baada ya wenzao wawili kutekwa nyara Mjini Mandera . Imethibitishwa kwamba wawili hao wameondoka kwenye Kaunti hiyo wekendi hii.
Kamishana wa Lamu Joseph Kanyiri, amepuuzilia mbali suala hilo akisema wawili hao wameitwa Jijini Nairobi kuhusu maswala ya kazi yao. Aidha amedokeza kwamba Lamu ni salama ikilinganishwa na Mandera.
Waziri wa afya kwenye Kaunti la Lamu Anne Gathoni, amethibitisha kwamba madaktari hao wamehama sehemu hiyo, lakini amekanusha madai kwamba kuondoka kwao hakuhusiani na swala la ukosefu wa usalama.
Tangu kutekwa nyara kwa madaktari wawili wa Cuba siku ya Ijumaa na kundi Al Shabab , madaktari wengine waliokuwa wakihudumu kwenye Miji za Wajir na Garissa wamelazimika kurejea Nairobi.