Serikali imeanzisha mikakati ya kudhibiti kilimo cha mahindi na bei ya unga wa ugali kufuatia kuchelewa kwa mvua ya kufanikisha upanzi wa mimea mwaka huu.
Akithibitisha kupokea malalamishi ya Wakenya wengi kuhusu ongezeko la bei ya unga wa mahindi, Waziri wa Kilimo Mwangi Kiunjuri amesema upungufu wa mahindi yanayoweza kukidhi hitaji la wananchi kutoka kwa wakulima wa humu nchini ndiyo sababu kuu inayoathiri bei ya unga.