Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Fearless, Trusted News
★★★★ - on Play Store
Download App

SRC kupunguza baadhi ya marupurupu kwa wafanyakazi wa umma

Katika hatua inayolenga kupunguza gharama ya kulipia mishahara ya wafanyakazi wa umma,  Tume ya Kuratibu Mishahara ya Wafanyakazi hao, SRC imeanza kuondoa baadhi ya marupurupu wanayopewa. SRC imesema inalenga kuondoa jumla ya marupurupu katika vitengo mia moja arubaini na kimoja. Katika awamu ya kwanza tume hiyo imesema kwamba itatathmini marupuruu ya nyumba, likizo na hali ngumu ya kufanyia kazi ili kuhakikisha usawa miongoni mwao, japo huenda yakasalia.

Aidha marupurupu katika vitengo vingine huenda yakaondolewa au kujumuishwa ili kukabili visa ambapo baadhi ya wafanyakazi wa umma wamekuwa wakijinufaisha. Inaarifiwa kuwa wafanyakazi wengi marupuruu hayo ni zaidi ya nusu ya mishahara wanayolipwa hivyo kuilazimu serikali kutumia fedha nyingi katika bajeti yake kuyatosheleza. Hatua hiyo huenda ikaibua mvutano mkali baina ya tume hiyo na wafanyakazi wa umma ambao kwa muda sasa wamekuwa wakipinga kupunguzwa kwa mishahara. Jumla ya wafanyakazi laki saba na hamsini wa serikali kuu, zile za kaunti na idara mbalimbali wanatarajiwa kuathirika na mpango huo.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902